85. Tunza Kumbukumbu Muhimu za Mahusiano ya Kiajira

Utangulizi

Ndugu msomaji wa makala za Uchambuzi wa Sheria ambapo tumekuwa tukiichambua Sheria ya Kazi. Katika makala zilizotangulia tumeangalia mambo mbalimbali yanayohusu sheria za kazi na namna zinavyoathiri mahusiano baina ya mfanyakazi na mwajiri. Tumeanza kujifunza kanuni mbalimbali ambazo mwajiri anapaswa kuzingatia pale anapokusudia kuajiri mfanyakazi. Katika makala iliyopita tulijifunza juu ya Kanuni 11 inayohusu na kumtaka mwajiri kulipa kiwango cha Mshahara kinachostahili.

Leo tunakwenda kuangalia Kanuni ya 12 katika mfululizo huu ambayo inamtaka mwajiri kutunza Kumbukumbu muhimu za Mahusiano ya Kiajira. Karibu tujifunze.

Tangu kuanza mfululizo wa makala hizi ya mambo muhimu ya ambayo mwajiri anapaswa kuzingatia pindi anapotaka kumwajiri mfanyakazi ilikuwa na lengo la kujifunza na kuweza kuhakikisha utunzwaji wa taarifa na kumbukumbu muhimu katika masuala ya ajira. Hivyo basi katika Kanuni hii ya 12 tunakwenda kuhitimisha mfululizo huu wa kanuni za kuzingatia katika kuajiri.

Kanuni ya 12

Tunza Kumbukumbu Muhimu za Mahusiano ya Kiajira

Sheria ya Ajira pamoja na mambo mengine imezungumzia suala la malipo ya kazi ambayo mwajiriwa anapaswa kulipwa kutokana na kazi anayoifanya.

Msingi wa kuangalia na kujifunza juu yataratibu za kuweza kuajiri mwajiriwa kwa mujibu wa Sheria za Ajira ni kuhakikisha taarifa muhimu zianzoainisha mahusiano ya kiajira zinapatikana kwa ufasaha kama sheria inavyoelekeza.

Sheria ya Ajira inampa wajibu mwajiri kuhakikisha anatunza kumbukumbu muhimu za mahusiano ya kiajira baina yake na mwajiriwa.

Kifungu cha 15 (1) (a) – (i), (5) cha Sheria ya Ajira kinaeleza;

  (1) Subject to the provisions of subsection (2) of section 19, an employer shall supply an employee, when the employee commences employment, with the following particulars in writing, namely-
name, age, permanent address and sex of the employee;
place of recruitment;
job description;
date of commencement;
form and duration of the contract;
place of work;
hours of work;
remuneration, the method of its calculation, and details of any benefits or payments in kind; and
any other prescribed matter.  
(5) The employer shall keep the written particulars prescribed in subsection (1) for a period of five years after the termination of employment.                    

Kwa tafsiri nyepesi kinaeleza ulazima wa mwajiri kumpatia maelezo ya maandishi mwajiriwa yenye kuhusu taarifa zake binafsi, mahali alipajiriwa, mahali pa kazi, maelezo/majukumu ya kazi, tarehe ya kuanza kazi, aina ya mkataba na muda wake, muda wa kazi, mshahara na ukokotoaji wake n.k

Mwajiri anawajibika kutuza kumbukumbu za kiajira kwa kipindi kisichopungua miaka 5 baada ya ukomo wa ajira.

Tunaona waajiri wengi hawana mfumo madhubuti wa utunzaji wa kumbukumbu za kiajira hivyo kusababisha mgongano usio wa lazima baina ya pande mbili.

Endapo mwajiri atashindwa kutunza kumbukumbu na suala au mgongano ukaibuka baina ya mwajiri na mwajiriwa basi mwajiri atalazimika kuleta kumbukumbu zinazohusu ajira.

Hitimisho

Ni muhimu sana kwa mwajiri pindi atakapoajiri mfanyakazi atengeneze mfumo wa kuweka na kutunza kumbukumbu za kiajira tangu kuajiriwa kwake na endapo kutakuwa na hatua za kinidhamu zozote zilizochukuliwa na mwajiri dhidi ya mwajiriwa. Hii itamsaidia mwajiri kuchukua hatua stahiki katika wakati mwafaka pindi patakapojitokeza mgongano wowote. Zaidi sana itamsaidia mwajiri kutobambikiwa madai na waajiriwa wasio waaminifu wanaotumia mwanya wa kutokuwepo kwa kumbukumbu sahihi za masuala ya kiajira.

Kumbuka ‘kutokujua sheria si utetezi iwapo utatenda kosa lolote tafuta maarifa sahihi ya kisheria yakusaidie kufanya maamuzi sahihi kila siku.

Nakutakia siku njema ndugu yangu.

Isaack Zake, Wakili

Mwandishi Isaack Zake ni wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania wa kujitegemea anayefanya katika ofisi za Uwakili Zake Advocates zilizopo Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed. Isaack Zake anatoa elimu ya kisheria, ushauri wa kisheria na usimamizi wa kisheria katika maeneo mbalimbali kama Sheria za Kazi, Mirathi, Ndoa, Mikataba na Biashara. Kwa ushauri usisite kuwasiliana naye kwa 0713 888 040 na email zakejr@gmail.com