Happy Birthday Uliza Sheria

Utangulizi 

Habari za leo ndugu yangu msomaji na mfuatiliaji wa mtandao wa Ulizasheria. Awali ya yote napenda kumshukuru Mungu kwa nafasi hii tuliyopewa leo kuadhimisha mwaka mmoja katika kazi ya kutoa elimu na ushauri kwa masuala ya kisheria.

Utakumbuka ndugu yangu msomaji mnamo tarehe 20th August 2017 tuliwakaribisha wote kufuatilia blog yetu hii ya uliza sheria.

Mtandao wa ulizasheria ulijiwekea malengo ya kutimiza ambayo yamekuwa dira ya kazi yetu kila mara.

Lengo kuu la mtandao huu.

  • Kutoa elimu ya msingi ya sheria kwa mwananchi wa kawaida kabisa ili apate kufahamu namna ya kuishi kwa mujibu wa sheria
  • Kutatua matatizo na kutoa majibu ya maswali ya jamii katika changamoto za kisheria wanazokumbana nazo kila siku.
  • Kusaidia lengo la Tanzania 2025 kuwa nchi yenye kuzingatia sheria na utawala bora.

Hakika kwa sehemu yetu tunasema tumefanya wajibu wetu kwa kadri tulivyoweza kwa kipindi cha mwaka 1.

Katika kipindi cha mwaka 1 tumeweza kuandika makala 205 za maeneo mbalimbali ya kisheria ikiwa ni pamoja na;

  • Makala za jumla
  • Katiba
  • Sheria za ardhi
  • Sheria za mikataba
  • Sheria za madhara
  • Sheria za ndoa
  • Sheria za mirathi
  • Sheria za makosa ya Jinai
  • Sheria za usalama barabarani
  • Sheria za Mtoto
  • Sheria za haki miliki
  • Sheria za Kazi

Kwa kipindi cha mwaka uliza sheria imeweza kufikia mikoa yote ya Tanzania ambayo tumepata wasomaji na wafuatiliaji wa mtandao wa ulizasheria. Tumepokea maswali kutoka kila upande wa Tanzania na hata nchi za nje wakitaka kujua ufafanuzi wa mambo mbalimbali ya kisheria.

Pia tumepokea simu kutoka vituo kadhaa vya redio vikitaka kujua ufafanuzi wa masuala ya kisheria na hata magazeti mbalimbali.

Haya yote ni mafanikio yetu sisi na wewe ndugu msomaji kwa kazi kubwa hii ambayo mpaka sasa tunaendelea kuifanya kwa pamoja.

Matarajio Yetu

Katika kuanza mwaka wa 2 wa huduma zetu kama ulizasheria tunatarajia kuweka nguvu na maarifa zaidi katika kushughulikia masuala mbalimbali ya kisheria yanayowatatiza wananchi na wadau wetu.

Aidha katika mwaka wa 1 tumetumia muda mwingi kuandika juu ya makala mbalimbali zinazotoka kwetu. Ni mipango yetu kwa mwaka huu wa 2 tuanze kuandaa makala zinazotokana na maswali ya wasomaji wetu kwa kadri inavyowezekana. Hii itasaidia zaidi kutatua changamoto ambazo zinawakumba wasomaji wa mtandao huu na hivyo kupelekea kutimizwa kwa lengo la kutatua matatizo ya kisheria wao wenyewe.

Tunatarajia kuboresha zaidi mfumo wa kupokea maswali hasa kwa njia ya sms, watsup au e-mail. Ni wazi kwamba tumekuwa na changamoto kubwa ya watendaji wa uliza sheria hivyo bado hatuwezi kujibu simu ya kila mmoja. Hivyo tutaandaa utaratibu mzuri wa kuweza kujibu maswali yako pasipo kuwa na ulazima wa kupiga simu. Endapo hitaji la simu au kuongea moja kwa moja na mwanasheria litahitajika basi utajulishwa utaratibu husika.

Tunatarajia kuanzisha siku ya ulizasheria ambayo tutakuwa tunaiadhimisha kila siku ya tarehe 20 mwezi wa Agosti ya kila mwaka, ambapo tutakutana na wadau wetu wa mtandao wa uliza sheria kwa lengo la kuwahudumia ana kwa ana.

Ni ahadi yetu kwako msomaji kukuletea suluhu ya kisheria katika maeneo mbalimbali ambayo blog yetu itaendelea kutoa huduma zake.

Nikutakie heri na fanaka ya kuadhimisha mwaka 1 wa mtandao wa uliza sheria.

Tunakukaribisha kwa maoni, mapendekezo, ushauri wa namna bora ya kuboresha huduma zetu kwa siku zijazo. Tafadhali wasiliana nasi kwa maelekezo yaliyoandikwa hapa chini.

Shukrani za kipekee

kwa namna ya kipekee ninapenda kukushukuru sana rafiki yetu, ndugu yetu na Kocha Dr. Amani Makirita kwa sehemu kubwa uliyofanya kufanikisha uwepo wa blog hii hata sasa. Kazi yako hii inawafikia watanzania na kuwagusa hata wengine walio nje ya nchi. Shukrani hizi ziwaendee pia wanamafanikio wa Kisima cha Maarifa haya ni mafanikio yetu sote. Tuendelee kuweka kazi na maarifa kila siku.

Mungu awabariki sana.

Wako

Isaack Zake

Mwandishi Isaack Zake ni wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania wa kujitegemea anayefanya katika ofisi za Uwakili Zake Advocates zilizopo Dar es Salaam, Mtaa wa Bibi Titi Mohamed. Isaack Zake anatoa elimu ya kisheria, ushauri wa kisheria na usimamizi wa kisheria katika maeneo mbalimbali kama Sheria za Kazi, Mirathi, Ndoa, Mikataba na Biashara. Kwa ushauri usisite kuwasiliana naye kwa 0713 888 040 na email zakejr@gmail.com